Toleo no: 33
08 January 2016
UMUHIMU WA KUTAMBUA KUSUDI III “Moyo wa mtu hufikiri njia yake; Bali Bwana huziongoza hatua zake ” Mithali 16:9 Katika biblia tafasiri ya kiingereza [NIV] mithali 16:9 inasema, “Moyo wa mtu hupanga
Weekend of purpose Season III
Dates: 09-10 April 2016,
mipango yake ili kufikia malengo yake, lakini Bwana huongoza hatua zake” (Tafsiri ya mwandishi). Hii inatupa kufahamu kuwa jukumu la kupanga mipango ili kufikia malengo fulani katika maisha yetu ni jukumu la mtu binafsi. Mpaka tumekuwa na mipango dhabiti katika kufikia
malengo tuliyonayo, Mungu hataongoza hatua zetu ili kufikia
malengo hayo. Akielezea umuhimu wa kuwa na mipango, na jinsi ambavyo Mungu huongoza hatua zetu ili kufikia malengo, kutimia kwa ndoto/maono, katika maisha ya mtu; mwenyehekima
Place: Boko Carmeli For more information call the following
mmoja amewahi kusema, “Ni vigumu kuongoza meli iliyosimama”. Mtu mwenye malengo au ndoto/maono katika maisha yake lakini hana mipango dhabiti ya kufikia jambo hilo, ni kama meli iliyosimama; hakuna namna nahodha ataweza kuiongoza meli hiyo; na hivyo hakuna namna meli hiyo itaweza kufika mwisho wa safari yake.
numbers; 0656211564 / 0652415516
Don’t miss IT
Jambo moja muhimu napenda ukumbuke; Kabla ya mipango hutangulia malengo. Malengo ni mambo unayotaka kuyafikia katika kipindi cha muda fulani; Mipango ni hatua na njia za kupita ili kufikia malengo hayo. Watu wengi wanashindwa kufanikiwa, si kwa sababu hawana uwezo wa kufanikiwa; ila ni kwa sababu hawajui wanataka kufanikiwa katika jambo gani hasa [specific targets]. Mtu asiye na malengo ni sawa na msafiri anaye safari kwenda mahali kusipojulikana. Mpaka umekuwa na malengo
mahususi, hauwezi kuwa na mipango dhabiti ya kukutoa hapo ulipo. Nakumbuka wakati ninaanza mwaka 2015, mojawapo ya malengo niliyokuwa nayo ni kuhakikisha ninasoma angalau kitabu kimoja kipya kila mwezi; na nikaweka
Page 2 mipango/mikakati ya kufikia lengo hilo. Mpaka mwaka unaisha nimefanikiwa kutimiza na kuvuka lengo hilo la kusoma angalau kitabu kipya kila mwezi; hii ni mbali na machapisho mbalimbali ninayosoma; ambapo kwa ujumla imeongeza maarifa, ufahamu, hekima na kupanua uelewa wangu juu ya mambo kadhaa. Kumbuka jambo hili; Ili kuishi maisha yenye ufanisi, ni muhimu kwa malengo yako kuendana na ndoto zako au maono au kusudi la Mungu juu maisha yako.
Kama
mojawapo ya malengo yako katika mwaka huu ni kuongeza au kukuza uhusiano wako
Weekend of purpose Season III
na Mungu, au kujijengea tabia na mwenendo fulani wa kimaisha au kurudi shule au kusoma hadi kufikia ngazi fulani, kuanzisha biashara/jambo fulani au kuboresha mahusiano yako katika eneo fulani; weka mipango ya kufikia lengo hilo. Mipango ni kama malighafi za kutengenezea bidhaa [malengo], tunapoanza mwaka huu mpya amua kupanga mipango na kuiweka mipango hiyo mbele za Mungu; na mwisho wa
yote utapata bidhaa kamili yaani kufikia malengo/ndoto na maono uliyonayo ndani yako kwa mwaka huu [Mithali 16:3].
Dates: 09-10 April 2016, Place: Boko Carmeli For more information call the following
Unapokuwa na malengo pamoja na mipango dhabiti; inakuwezesha kuweka vipaumbele
numbers;
vyako vizuri juu ya matumizi yako ya fedha, rasilimali ulizonazo, muda wako na aina ya
0656211564 /
watu unaotaka kutumia nao muda wako; kama mtu hakusaidii kufikia malengo yako ni
0652415516
vizuri ukapunguza matumizi ya muda wako kwake. Kumbuka; watu wanaosafiri kwenda mahali kusikojulikana hupenda kusafiri pamoja na
watu wengine; watu wasiotaka kufikia malengo yoyote katika maisha yao, hupenda kila mtu afanye kama wao.
Life Minus Regret Program P.O. Box 66678 Dar Es Salaam Phone:0766-006040/ 0788-230333/ 0652-415516/ 0766-234156 Blog: lifeminusregret.blogspot.com Email:
[email protected]
Don’t miss IT