GOMBO LA WIKI/MWEZI Tuandikie au tuma ujumbe mfupi wa simu kupitia:
[email protected] www.facebook.com/mwlsamwelmkumbo +255 753 204 743
HUZUNI YA JINSI YA MUNGU
Mwl; Samwel Mkumbo
GOMBO LA WIKI
Na: Samwel Mkumbo Sehemu ya 3.
“HUZUNI YA JINSI YA MUNGU” Katika wiki hii tunaendelea na mtiririko wa kujifunza somo linaloitwa “HUZUNI YA JINSI YA MUNGU”, na wiki iliyopita tulijifunza mambo kadhaa, na mstari wetu mkuu tunaoutumia katika Somo hili ni ule wa 2 Wakorintho 7:10 na katika huo tutajifunza mengi zaidi…….. KARIBU!! 2 Wakorintho 7:10, umeandikwa hivi; “Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.” Wiki iliyopita katika sehemu ya pili tulitazama suala la KUKIRI DHAMBI, na naamini kwa jinsi tulivyolitazama kwa undani utakuwa umepata jambo la kukusaidia. Sasa baada ya hatua tulizokwisha kuzitazama. Tuendelee, na kumbuka haya ninayokufundisha ndiyo yatakayokuja kutusaidia nitakapokuwa nakuonesha TOFAUTI YA HUZUNI YA JINSI YA MUNGU, na ile HUZUNI YA DUNIA.
Kutubu dhambi. Kwa maneno rahisi ni kuamua/ kukata shauri kwa kuamua kubadili njia ambayo ulikuwa unapita katika maisha yako au jambo Fulani maishani mwako, nah ii inatokana na njia au hatua nilizokuelezea nyuma kupita. Yaani ili mtu afikie hatua hii ya Kutubu dhambi au kosa ni lazima kwanza awe AMELITAMBUA KOSA/DHAMBI yenyewe, kisha KUJUTUTIA halafu tena KUKIRI ndiposa KUTUBU HUFUATA. Lakini zaidi ya hayo niliyokwisha kukueleza hapo juu, natamani nikuongezee jambo ya kwamba kwa ujumla wake wa hayo niliyokufundisha katika sehemu mbili zilizopita, ni kwamba KUTUBU huja kutokana na KUKUBALI NA KUTII. Hayo ndiyo maelezo mafupi yanayoweza kumeza mambo mengi niliyokuandikia hapo juu, ni kwamba KUTUBU ni matokeo ya KUKUBALI na KUTII. Na labda ngoja nikueleze maana ya Kukubali na Kutii.
Kukubali Maana ya haraka ya neno “Kukubali” Ni kuwa tayari kufundishwa na BWANA ili upate ufahamu. hii inanipa uwezo wa kukwambia kuwa jambo la msingi ili upate kufundishwa na upate ufahamu ni kuwa tayari kufundishwa na huyo anayekufundisha huko ndiko kunaitwa kukubali na ndiko kunaleta mabadiliko ya ndani na ya nje kwa mtu yeyote Yule. Isaya 48:16-17 inasema hivi; “16Nikaribieni, sikieni haya; tokea mwanzo sikunena kwa siri; tangu yalipokuwapo, mimi nipo; na sasa Bwana MUNGU amenituma, na roho yake.17 Bwana, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Sasa nataka nikuoneshe maneno haya;..,……. 16 Nikaribieni, sikieni haya;…… Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye…………. Mungu anaanza na neno NIKARIBIENI, maana yake ni wito anaokuita, kabla Mungu hajakufundisha kwanza anakuita mana hawezi kukufundisha ukiwa umezagaa zagaa tu au uko mbali nae, au uko katika hali ya kuhangaika. Huwa kwanza anakuita anasema NIKARIBIE, kisha anaongeza neno la msingi ambalo linaashiria “Utulivu”, pale anaposema SIKIENI HAYA… anachotaka kwanza ni utulivu wa mtu. Sasa mtu Yule anayetenda yote haya, yaani ANAEKARIBIA (kusikia wito/mwaliko) halafu ASIKIE HAYA….(anayetulia) ndiye anayepata nafasi ya KUFUNDISHWA NA BWANA, na huko ndiko tunaita KUKUBALI. Baada ya kukueleza hilo, nataka nikutazamishe jambo kidogo ili ujue zaidi juu ya kufundisha na BWANA. Zaburi 32:8 tunakuta maneno haya; “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;……..” sasa kwa hali ya kawaida neno kufundisha lina maana ya “Kupewa Maelekezo juu ya jambo Fulani”. Hivyo Mungu anaposema “Nitakufundisha” maana yake “Nitakupa maelekezo”. Sasa basi ikiwa nimekwambia KUTUBU ni matokeo ya Kukubali na Kutii ina maana Kutubu ni matokeo ya Kuwa tayari kufundishwa/Kupewa maelekezo na Kutii., (nitakuambia maana ya kutii mbele kidogo). Basi kwa maelezo mafupi tunaweza kusema mtu anapofikia hatua ya Kutubu ni lazima hapo nyuma “Alikubali kufundishwa/kupewa maelekezo na Akatii hayo”. Mtu anapofundishwa itamwezesha kufanya au kutokufanya hatua inayofuata yaani Kutii. Kutii
Ni kufanya kile ulichoamriwa baada ya kufundishwa, yaani baada ya kukubali kufundishwa ambapo nilikwambia ni Kupewa maelekezo, sasa ile hali ya kufanya jambo kama umepewa maelekezo ya kufanya au kutofanya jambo kama umepewa maelekezo ya kutofanya ndio inayoitwa Kutii. Luka 5:5 inasema hivi; Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu. Kauli anayosema Simoni inaweza kutupa mtazamo halisi wa hili ninalokufundisha hapa, tazama maneno haya “……… lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu. Simoni anachoonesha ni kwamba kitendo chake cha kushusha nyavu ni matokeo ya maelekezo aliyoyapata kutoka katika “NENO LILILOSEMWA NA YESU”, ahaa, hivyo basi Yesu angemwambia “asishushe nyavu” ni kweli asingeshusha maana kwa wakati huo alikuwa anategemea Neno toka kwa Yesu ili Atii. Yohana 5:8-9 inasema; Yesu akamwambia, Simama, jitwike godoro lako, uende. akawa mzima, akajitwika godoro lake, akaenda…………….
9
Mara yule mtu
Sasa labda nikupe maelezo ya kina hapa katika habari ya Kutii, mara nyingi kutii hutokea wakati mtu anapoambiwa aua anapopewa maelekezo ya kufanya jambo ambalo kwa akili ya kawaida(kibinadamu) au ufahamu wake inakuwa kama haiwezi kuwa. Na ndio maana huyo mtu (katika Yohana 5:8-9) kama ukianzia kusoma tangu mistari ya mwanzoni ni mtu aliugua kwa miaka mingi, na hakuweza kupona na imani ya kupona kwake aliiweka kwenye maji ya birika. Lakini Yesu alipokuja aliibadilisha na hivyo huyu mtu alihitajika kuwa na Utii. Ahaa, sasa basi hii tunaweza kuileta hata katika habari ya “kutubu” Kutii kunahitajika maana unaweza kupewa maelekezo kwa kufundishwa yanayokutaka uache au usitende jambo ambalo kwa hali ya kawaida (kibinadamu) unaweza kuliona si Tatizo hatakidogo wala halina shida. NA HAPO NDIPOSA MUNGU HUTUMIA HUZUNI ILIYO YA JINSI YA MUNGU ILI KUWEKA NGUVU ITAKAYOKUKIMBIZA KUTUBU. Tazama nami: “Huzuni ya Jinsi ya Mungu” ni matokeo ya Kutambua, Kujutia na Kukiri Kosa lakini ili ikamilike zaidi Huzuni ya Jinsi ya Mungu hukupeleka “Kutubu” maana katikati ya Huzuni ya Jinsi ya Mungu kuna maelekezo (mafundisho) yanayokuja yatakayokuhitaji uyatende na unapoyatenda ndio kutii na hayo maelekezo
hayatakupelekea mahali pengine kama ni suala linalohusu Dhambi/Kosa zaidi ya kukutaka “Utubu”. Na hiyo ndiyo tofauti kubwa nitakayokueleza hapo mbele, kati ya “Huzuni ya Jinsi ya Mungu” na ile ya Dunia. Tazama nami tena: Huzuni ya Dunia haiwezi kukupeleka mwisho mzuri, haiwezi kukufanya uangalie kuwa kuna tumaini tena pale unapokuwa katika hali ngumu na ya dhiki, ndio! Huzuni ya Dunia haiwezi kukufanya utazame kuwa kuna Mungu, ila inakufanya Uone kuna MUNGU aliyejiandaa kuhukumu tu na wala si kusamehe. Huzuni ya Dunia inakufanya uone ulilolifanya limekuangamiza wala hakuna njia tena, wala hakuna kutoka tena, kama ni hali ya umasikini, huzuni ya dunia itakuambia ulipokataa kutoa rushwa ili upate kazi ulikosea, kama ni binti itakuambia kutovaa mavazi yanayoonyesha mwili wako ndio kumekufanya usiolewe hata leo, kama ni magonjwa huzuni ya dunia itakwambia ulipokataa kwenda kwa mganga ndio umejiangamiza, ujumla wa yote hayo ni MAJUTO na majuto HULETA MAUTI …… bali huzuni ya dunia hufanya mauti.” (2 Wakorintho 7:10) HIYO NDIO HUZUNI YA DUNIA, ITAENDELEA…………