GOMBO LA WIKI/MWEZI Tuandikie au tuma ujumbe mfupi wa simu kupitia:
[email protected] www.facebook.com/mwlsamwelmkumbo +255 753 204 743
HUZUNI YA JINSI YA MUNGU
Mwl. Samwel Mkumbo
GOMBO LA WIKI
Na: Samwel Mkumbo Sehemu ya 1.
“HUZUNI YA JINSI YA MUNGU” Katika GOMBO LA WIKI hii ninakufundisha kuhusu “HUZUNI YA JINSI YA MUNGU”, na hii ni kutokana na swali nililoulizwa na ndugu mmoja kutokana na kitabu cha 2 Wakorintho 7:10, umeandikwa hivi; “Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.” KARIBU!! Inawezekana si Neno geni kwako kusikia “HUZUNI YA JINSI YA MUNGU” na inawezekana kwako ni geni pia jambo hili lakini sote tulete mawazo yetu hapa! Weka moyo wako kwenye Utulivu ili nikufundishe na Roho Mtakatifu aseme nawe juu ya hili KWA JINA LA YESU, Neno Hili Likawe Na Nguvu Na Lenye Kuponya KWA JINA LA YESU Na Kuleta Hekima Ndani Yako KWA JINA LA YESU. Aaamen Ili kuweza kuyatenda mapenzi ya Mungu ni muhimu kuyajua na ili kuyajua mapenzi yake basi yanapatikana kwa kulijua Neno lake, naam!, Neno ndilo limebeba maelekezo ya Mungu, sasa basi moja ya jambo Mungu ameliweka bayana ni pale mwanadamu anapokosea ni KUTUBU na KUREJEA, naam, ni “Kutubu na Kurejea”. 37
Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu ( Matendo 2:3738) Kabla sijaendelea kukueleza mengi labda nikupe maelezo haya kwanza, TOBA ni “Tokeo” yanayoleta “Matokeo”, naam! Ni sahihi, na nirudie tena kukazia hapo Toba ni TOKEO LINALOLETA MATOKEO. Na hii ni kwa sababu kabla “Toba” haijafanyika kuna mambo” Yanayootangulia” na baada yake kuna mambo “Yanayofuata” ndio maana ni kasema kuwa……. Toba ni Tokeo linaloleta Matokeo……., na hiyo ni muhimu kuijua sana sana maana ..,,…,..tunaweza tusithamini toba kwa maana hatujui matokeo yake, lakini pia ,,..,,..,,tunaweza tusithamini toba kwa kuwa hatujui inasababishwa na nini……… lakini pia tunaweza kuifanya kwa mazoea kwa kuwa hatujui inatokana na nini na itazaa nini.
Lakini katika Somo hili nitasimama kwenye upande wa kukufundisha KUTUBU kama TOKEO lililotokea kutokana na mambo kadhaa. Matendo 2:37 inasema hivi; 37
Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Katika mstari huo tunaona jinsi gani unaweza kuona kwamba Kutubu ni Tokeo linalokuja baada ya mambo kadhaa kutokea na mojawapo tumeliona hapo juu, biblia inanena hivi……37Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao.,..,…”
MAMBO YANAYOTANGULIA ILI TUPATE KUTUBU Kuna mambo kadhaa yanayotangulia ili kutupa Nguvu na Wito wa kutubu na haya ni muhimu kuyafahamu maana kwa kutojua haya wengine wameishia kutojua nini cha kufanya yanapotokea katika maisha yao ya kila siku, na wengine yamewatokea wakaishia kwenye hayo pasi kwenda hatua iliyo ya muhimu ambayo ni “Kutubu”
Kutambua dhambi /kosa Hili ndilo jambo la kwanza aambalo huleta matokeo ya kutubu juu ya jambo lolote lile, nah ii inatupa kuelewa zaidi pale ninapikwambia Kutubu ni Tokeo, na moja ya sababu ya tokeo hilo ni “Kutambua Kosa” ambalo mtu au watu wanakuwa nalo. Kwa habari ya Mfalme Daudi katika Zaburi 51:3 tunasoma maneno haya: “Maana nimejua mimi makosa yangu ,na dhambi yangu i mbele yangu daima ". Daudi anasema kwa Mungu kuwa jambo linalompa Kutubu au jambo lilimpelekea kwenda kwa Mungu kuomba msamaha analisema hivi “…. Maana NIMEJUA mimi MAKOSA yangu……” Watu wengi tumekuwa hatupati msamaha wa dhambi kwakuwa hatuko tayari “Kutubu” na hii ni kwasababu hatuna utayari na hatutaki “Kutambua” dhambi zetu. Kosa letu ni kuwa tunarahisisha dhambi na kufanya kuwa ni jambo la kawaida, na mara nyingi kwa mawazo na maneno yetu au hata matendo yetu tumehalalisha haramu na kuharamisha halali NI MBAYA. Ni muhimu kuelewa kwamba unapojikuta “Umetambua” ya kuwa unalo kosa mbele za Mungu ni nafasi yako ya kwenda Kutubu na pia ukiona unapata hamu ya Kutubu basi ujue ndani kama nje bado hujaona jua tu roho yako imetambua kuna kosa
mahali na ndio maana unapata hamu ya kutubu usianze kufikiri-fikiri anza Kutubu na utaona jinsi Mungu anavyolifunua hilo ulilolitambua rohoni.
Kujutia dhambi. Ili mtu aweze kujutia dhambi ni lazima kuwepo na mguso wa ndani ya moyo (nafsi yake), lakini hii si hatua ya mwisho, maana wengi wanapotoka hatua ya kwanza (Kutambua Kosa) huwa wanaishia kwenye hii hatua ya pili ya “Kujutia” lile alilolitambua kuwa ni kosa ndani yake na huwa wanaishia hapo, Luka 15:17 utakuta maneno haya:Alipozingatia moyo mwake alisema ……………….. mwana mpotevu hakuwa na chakufanya baada ya kutambua dhambu yake ila kwanza kujutia moyoni. NAHATUWEZI KUJUTIA DHAMBI BILA YAKUITAMBUA DHAMBI. Itaendelea,…….. Mungu awe pamoja nawe katika wiki hii unapotafakari GOMBO LA WIKI.